Aussems amesema amefarijika kuona mashabiki wakijitokeza kwa wingi uwanjani jana lakini zaidi juzi Simba ilipotua mkoani Mara
“Tumefarijika na mapokezi waliyotupa mashabiki wa hapa ikiwa ni muda mrefu umepita tangu Simba ije kucheza hapa,” amesema
“Tumewaachia zawadi ya ushindi, sisi tunaelekea Dar ambako tutacheza mchezo mmoja Jumanne (na JKT Tanzania) kisha tutaelekea mkoani Mbeya kuzikabili Mbeya City na Tanzania Prisons”
Msafara wa Simba ulilala jijini Mwanza ambapo leo wanarejea jijini Dar es salaam kwa usafiri wa ndege