Wanaosema Simba ‘inabebwa’ wajitafakari

Afisa Habari wa Simba Haji Manara amewashangaa mashabiki wanaosema klabu hiyo inabebwa na waamuzi wakati timu hiyo imepata mafanikio nje na ndani ya Tanzania kutokana na ubora wa kikosi chake

Manara amesema Simba imekuwa ikicheza kila baada ya siku mbili na inapata matokeo kutokana na ubora wake na si vinginevyo

“Tumefika robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa tulibebwa na nani?” alihoji Manara

“Hata hao Yanga ambao mashabiki wao wanalalamika kuwa tunabebwa nao tuliwafunga, je tulibebwa?”

“Kwa sasa Simba ndio timu yenye kikosi bora Tanzania, ndio mabingwa watetezi na baada ya wiki moja tutakuwa kileleni mwa msimamo wa ligi tayari kurejesha ubingwa Msimbazi”

Simba imebakisha michezo 11, lakini inahitaji kushinda michezo nane tu ili iweze kutwaa ubingwa

Aidha kama Yanga itashindwa kuifunga Azam Fc kesho, Simba itahitaji kushinda michezo miwili tu ili kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi