Simba kushirikiana na Porto FC

Mwekezaji wa klabu ya Simba Bilionea Mohammed Dewji ‘Mo’ akiwa nchini Ureno alitembelea kitua cha kulelea vipaji cha klabu ya Porto Fc

Ziara yake hiyo ilikuwa mahsusi kwa ajili ya kutafuta fursa ya ushirikiano baina ya klabu ya Porto Fc na Simba

“Jana nilipata nafasi nzuri ya kujifunza nilipoitembelea @FCPorto ambapo niliweza kujua fursa za ushirikiano kwa kituo cha kukuzia vipaji cha Simba huko mbeleni,” amebainisha Mo

“Tuna mengi ya kujifunza na kupata kutokana na uzoefu wa Porto FC. Natarajia kuimarisha mazungumzo yetu hivi karibuni”

Hii ni habari njema kwa Simba ambayo ina mipango ya kujenga mifumo imara itakayoinufaisha klabu hiyo siku za mbeleni