Zana aipa mtihani Simba

Licha ya ubora wake hasa wakati timu ikishambulia, beki wa kulia wa Simba Zana Coulibaly ameonesha kuwa na mapungufu hasa wakati timu inapokuwa inashambuliwa
Katika michezo ya hivi karibuni, Zana aliyetua Simba wakati wa usajili wa dirisha dogo, ameonekana kutotimiza vyema majukumu yake katika ulinzi

Na hiyo imekuwa sababu ya mashabiki wengi wa Simba kuulizia hali ya Shomari Kapombe ambaye licha ya kuanza mazoezi mepesi, kuna uwezekano mdogo kwake kurejea dimbani msimu huu kutokana na muda uliobaki kuwa mdogo kabla ya ligi kumalizika

Katika mchezo dhidi ya JKT Tanzania, kocha Patrick Aussems alilazimika kumfanyia mabadiliko Zana kwenye kipindi cha pili nafasi yake kuchukuliwa na Nicholas Gyan

Inaelezwa Zana alipata majeraha ya goti

Zana alisajiliwa kuongeza nguzu pembeni baada ya Kapombe kupata majeraha wakati akitimiza majukumu ya timu ya Taifa nchini Afrika Kusini

Hata hivyo Simba huenda ikalazimika kufanya uamuzi mgumu wakati wa usajili kwa kuachana na mmoja kati ya Zana au Gyan anayeonekana kupoteza nafasi katika kikosi cha kwanza