Kesi ya kupinga uchaguzi Yanga yafutwa, kadi zote kutumika

Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi ya TFF Malangwe Mchungahella ambaye Kamati yake inashirikiana na kamati Maalum ya Uchaguzi ya Yanga, amesema kesi iliyokuwa imefunguliwa na Wanachama wawili ya kupinga uchaguzi wa Yanga, imefutwa.

Mchungahella amesema baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kufuta shauri hilo, uchaguzi utafanyika May 05 kama ulivyopangwa

Aidha amesema mpaka sasa zoezi la kampeni linaendelea vizuri na hakuna malalamiko yoyote ya uvunjwaji wa sheria

Mchungahella amesema wanachama wote wenye kadi za zamani (kitabu) na za ki-elektroniki (posta) wataruhusiwa kushiriki katika mchakato huo

Muhimu ni Mwanachama lazima awe amelipia ada ya mwaka