Yondani aongeza nguvu Yanga

Beki kisiki wa Yanga Kelvin Yondani amejumuishwa kwenye kikosi cha timu hiyo kilichoondoka leo kuelekea mkoani Iringa kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali kombe la FA dhidi ya Lipuli Fc

Mchezo huo utapigwa Jumatatu, May 06 katika uwanja wa Samora

Yondani amemaliza kutumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar uliopigwa jijini Mwanza

Amekosa michezo dhidi ya Mtibwa Sugar, Azam Fc na Tanzania Prisons

Wachezaji waliojumuishwa kwenye msafara huo ni pamoja na Klaus Kindoki, Ramadhan Kabwili, Kelvin Yondan, Haji Mwinyi, Juma Abdul, Paul Godfrey, Abdallah Shaibu, Endrew Vicent, Said Makapu, Feisal Salum, Mohammed Issa, Papy Tshishimbi, Thaban Kamusoko, Deus Kaseke, Mrisho Ngasa, Ibrahim Ajib, Raphael Daud, Herieter Makambo, Amiss Tambwe, Haruna Moshi, Jaffar Mohamed, Ibrahim Hamid na Pius Buswita

Mchezo wa kwanza wa nusu fainali kombe la FA unapigwa leo kati ya Azam Fc dhidi ya KMC, saa moja jioni uwanja wa Azam Complex