Igangula ajitoa uchaguzi Yanga

Mgombea mwingine wa nafasi ya Mwenyekiti Baraka Igangula amejiondoa katika kinyan’ganyiro cha nafasi hiyo katika uchaguzi wa Yanga utakaofanyika kesho Jumapili

Inaelezwa Igangula ameamua kumuunga mkono Dk Mshindo Msolla ambaye sasa atachuana na Dk Jonas Tiboroha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Yanga

Dk Msolla amepata uungwaji mkono mkubwa na anapewa nafasi kubwa ya kuibuka kidedea kwenye uchaguzi huo wa kesho