
Yanga ina alama 80 na imebakiwa na michezo minne ambayo hata kama wakishinda yote watafikisha alama 92
Simba yenye alama 75 ikishinda michezo sita itafikisha alama 93 ambazo hazitafikiwa na timu nyingine yoyote
kesho Simba itarejea uwanja wa Sokoine kusaka alama nyingine tatu kati ya 18 zinazohitajika ili kutetea ubingwa katika mchezo dhidi ya Tanzania Prisons
Habari njema ni kwamba baada ya mchezo huo, Simba itarejea jijini Dar es salaam ambako itacheza michezo sita
Ushindi katika michezo hiyo itakayopigwa uwanja wa Taifa/Uhuru, utawahakikishia mabingwa hao kuubakisha ubingwa Msimbazi mapema tu hata kabla ya tarehe ya mwisho ya kufunga msimu