Simba iheshimiwe – Manara

Msemaji wa Simba Haji Manara ameeleza kushangazwa na kauli zinazotolewa na baadhi ya makocha wa timu zinazoshiriki ligi kuu kuwa timu hiyo inabebwa

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Mbeya leo, Manara amesema uongozi wa timu hiyo uliamua kukaa kimya kwa kuwa haukuona umuhimu wa kuwajibu wanaoropoka

Hata hivyo amesema ukimya huo haumaanishi kuwa wanazifurahia kauli hizo

Amesema Simba ni taasisi kubwa na ametaka taasisi hiyo iheshimiwe, isiingizwe katika tuhuma ambazo hazina ukweli wowote

“Tunawataka wote wanaotuhusisha na masuala ya rushwa waache mara moja na kama wana usahidi wapeleke kwa vyombo husika,” amesema

“Simba sio klabu dhaifu, Simba sio klabu nyonge isifike mahali Simba ikafanywa kuwa ni timu dhaifu. Simba ni taasisi kubwa, tunaomba iheshimiwe”

“Mafanikio tunayopata yanatokana na ubora wa timu yetu. Msimu huu tumefika robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa, mtu anasemaje kuwa kiwango cha soka Tanzania hakijapanda?”

“Huku ni kuikosea heshima nchi yetu”