
Kagera Sugar inayonolewa na kocha Mecky Mexime tayari kimewasili jijini Dar es salaam kusubiri mchezo dhidi ya Simba utakaopigwa Ijumaa, May 10
Simba wao watarejea jijini Dar es salaam leo wakitokea mkoani Mbeya ambako walifanikiwa kuchukua alama zote sita dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons
Hata hivyo kabla ya kucheza na Kagera Sugar Ijumaa, siku ya Jumatano Simba itachuana na Coastal Union katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa/Uhuru
Simba inahitaji kushinda michezo mitano tu kuweza kutetea ubingwa wake bila ya kujali matokeo ya Yanga ambayo imebakiwa na michezo minne ambayo kama wakishinda yote watafikisha alama 92
Ushindi katika michezo mitano utaifanya Simba ifikishe alama 93