Kagera Sugar yawahi Dar, Simba kurejea leo kutoka Mbeya

Kagera Sugar ndio timu pekee iliyopata ushindi dhidi ya Simba katika michezo minne ya kanda ya ziwa waliyocheza mabingwa hao watetezi kwenye duru ya pili

Kagera Sugar inayonolewa na kocha Mecky Mexime tayari kimewasili jijini Dar es salaam kusubiri mchezo dhidi ya Simba utakaopigwa Ijumaa, May 10

Simba wao watarejea jijini Dar es salaam leo wakitokea mkoani Mbeya ambako walifanikiwa kuchukua alama zote sita dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Hata hivyo kabla ya kucheza na Kagera Sugar Ijumaa, siku ya Jumatano Simba itachuana na Coastal Union katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa/Uhuru

Simba inahitaji kushinda michezo mitano tu kuweza kutetea ubingwa wake bila ya kujali matokeo ya Yanga ambayo imebakiwa na michezo minne ambayo kama wakishinda yote watafikisha alama 92

Ushindi katika michezo mitano utaifanya Simba ifikishe alama 93