TFF yapongeza uongozi mpya Yanga

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia amewapongeza Viongozi wapya wa Klabu ya Young Africans kwa kuchaguliwa kuiongoza klabu hiyo kwa kipindi cha miaka minne (4)

Karia amesema TFF itashirikiana na Viongozi hao katika maendeleo ya Mpira wa Miguu nchini

Wanachama wa Yanga jana walikamilisha salama mchakato wa uchaguzi wa klabu hiyo kwa kuwachagua Dk Mbette Mshindo Msolla kuwa Mwenyekiti na Fredrick Mwakalebela kuwa Makamu Mwenyekiti pamoja na kuchaguliwa kwa wajumbe wengine nane wa Kamati ya Utendaji