Zahera ataja sababu ya Ngasa kukosekana mchezo dhidi ya Ruvu Shooting

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema winga Mrisho Ngasa hakuweza kucheza jana mchezo dhidi ya Ruvu Shooting baada ya kuugua ghafla

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo, Zahera alisema Daktari wa timu Dk Bavu alishauri mchezaji huyo asitumike kwenye mchezo huo hivyo kuamua kumtumia Paulo Godfrey ‘Boxer’ wingi ya kulia

“Ngasa alipata matatizo muda mfupi baada ya kuwa tumepata kifungua kinywa. Alianza kutapika mfululizo na baada ya kupatiwa huduma na Daktari wa timu Dk Bavu, alishauri asicheze,” alisema Zahera

Akizungumzia mchezo huo ambao Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0, Zahera aliwapongeza wachezaji wake kwa ushindi huo huku akifichua hawakuwa wamefanya mazoezi tangu walipocheza na Biashara United May 10

“Tulipata changamoto ya usafiri kutoka Mwanza hali iliyopelekea tuchelewe kurudi jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo. Hata baada ya kurudi tulilazimika kuwapa wachezaji mapumziko kwani walikuwa wamechoka”

“Nilifahamu mchezo wa leo (jana) hautakuwa mwepesi kwetu, lakini nimefurahi tumeweza kutumia moja ya nafasi tulizotengeneza ingawa tulikuwa na uwezo wa kufunga mabao zaidi kwenye kipindi cha kwanza”

Leave a comment