Kadi za njano zamuumiza Fei Toto

Kiungo wa Yanga Feisal Salum ‘Fei Toto’ ni miongoni mwa wachezaji wanaoongoza kwa kupewa kadi za njano msimu huu

Fei Toto tayari amekosa michezo mitatu ya ligi inayotokana na adhabu za kadi za njano

Kiungo huyo aliyesajiliwa na Yanga akitokea JKU ya Zanzibar, hafurahii kadi hizo kwani zinamharibia jina na kumpa sifa mbaya

Fei Toto amesema anachokifanya uwanjani ni kutimiza wajibu na maelekezo anayopewa na Mwalimu.

Anaamini baadhi ya kadi anastahili lakini yapo matukio ambao anadhani hatendewi haki na waamuzi

Aidha kiungo huyo amesema amekuwa akikamiwa na wachezaji wa timu pinzani hali inayomfanya acheze kwa presha kubwa

“Baadhi ya mechi huwa nakamiwa, na kunifanya nicheze kwa presha kubwa. Siwezi kusema uwezo wangu ndio chanzo cha kukamiwa kwani naamini kila timu inaingia uwanjani ikiwa na lengo la kupata alama tatu,” amesema

Leave a comment