Simba yapania kuweka sawa hesabu za ubingwa leo

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba leo wanashuka dimba la Uhuru kuwakabili Mtibwa Sugar katika mchezo ambao vijana wa Patrick Aussems wamepania kuchukua alama zote tatu

Baada ya kukosa ushindi katika michezo miwili iliyopita, Simba leo inahitaji ushindi ili kuweka sawa hesabu za ubingwa

Simba inahitaji alama saba kutoka michezo mitano iliyobaki kuweza kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

Kama itashinda leo, halafu ikashinda mchezo dhidi ya Ndanda Jumapili, sare au matokeo ya ushindi mchezo dhidi ya Singida United, yatatosha kuipa Simba ubingwa wa pili mfululizo

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema wachezaji wa timu hiyo wako katika hali nzuri kuelekea mchezo huo ambao wamepania kuondoka na alama zote tatu

Leave a comment