Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems ameeleza furaha yake baada ya timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Uhuru
Akizungumza na Wanahabari baada ya mchezo huo, Aussems amesema Simba ilitawala mchezo na ilistahili kuondoka na ushindi mnono
Aidha Aussems amesema ushindi umezidi kuisogeza Simba karibu na ubingwa wa pili mfululizo
“Tulitawala mchezo, tulitengeneza nafasi na tulifanikiwa kufunga. Jambo muhimu tumekaribia lengo letu,” amesema Aussems