Tarehe kama ya leo miaka saba iliyopita, May 17 2012 klabu ya Simba ilipatwa na majonzi makubwa baada ya kumpoteza kiungo wake Patrick Mafisango aliyefariki kwa ajali ya gari
Umauti ulimfika Mafisango kupitia ajali ambayo katika jitihada za kunusuru maisha ya mwendesha pikipiki, gari yake iliingia mtaroni na kusababisha apoteze maisha kutokana na majeraha aliyopata
Kabla ya kuja Tanzania Mafisango alichezea APR ya Rwanda na alipofika nchini alijiunga na Azam Fc kabla ya kusajiliwa na Simba
Mechi ya mwisho Mafisango kuichezea Simba ilikuwa dhidi ya Al Ahly Shandy nchini Sudan katika hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho, ambayo Simba ilitolewa kwa penalti 9-8, kufuatia sare ya jumla ya 3-3.
Hadi anafariki dunia, Mafisango alikuwa ni tegemeo Simba katika safu ya kiungo
Pamoja na kucheza kama kiungo, Mafisango pia anamudu kucheza nafasi ya beki wa kushoto na beki wa kati