John Bocco, Meddie Kagere na Emmanuel Okwi wameteuliwa kuwania tuzo ya mshambuliaji bora wa mwaka
Bocco, Kagere na Okwi wameongoza vyema safu ya ushambuliaji ya Simba wakifunga mabao 50 kati ya 72 yaliyofungwa kwenye ligi

Kagere anaongoza mbio za kuwania kiatu cha dhahabu ligi kuu ya Tanzania Bara akiwa amefunga mabao 20
Mshambuliaji huyo pia ndiye kinara wa mabao wa kikosi cha Simba katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika ambayo Simba imetolewa hatua ya robo fainali amefunga mabao sita
Bocco na Okwi wamefunga mabao 15 kila mmoja kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara
Kupiga kura tembelea tovuti rasmi ya MO SIMBA AWARDS kwa kubonyeza HAPA