Klabu ya Simba inaendelea na mchakato wa kuhuisha mikataba ya wachezaji wake ambayo inamlizika na tayari imemalizana na nahodha wake John Bocco
Taarifa za uhakika ni kwamba Bocco amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kukipiga Msimbazi hadi mwaka 2021
Bocco aliyeifungia Simba mabao 15 kwenye ligi ya Tanzania Bara msimu huu, alikuwa akiwaniwa na timu yake ya zamani Azam FC
Azam Fc inadaiwa kuwashawishi Aishi Manula, Erasto Nyoni, John Bocco na Shomaria Kapombe wasaini kunako klabu hiyo waliyokuwa wakicheza kabla ya kusajiliwa na Simba mwaka juzi
Msimu uliopita Bocco aliibuka kuwa mchezaji bora wa Simba na msimu huu ameteuliwa kuwania tuzo hiyo sambamba na Meddie Kagere na Clatous Chama
Zoezi la kuchagua mchezaji bora wa msimu huu tayari limeanza, kura zinapigwa kupitia tovuti rasmi ya Mo Simba Awards
Bonyeza HAPA kumpigia kura Bocco kama unadhani anastahili kuwa mchezaji bora wa Simba msimu huu