SIMBA Yamalizana na Bocco

Klabu ya Simba inaendelea na mchakato wa kuhuisha mikataba ya wachezaji wake ambayo inamlizika na tayari imemalizana na nahodha wake John Bocco

Taarifa za uhakika ni kwamba Bocco amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kukipiga Msimbazi hadi mwaka 2021

Bocco aliyeifungia Simba mabao 15 kwenye ligi ya Tanzania Bara msimu huu, alikuwa akiwaniwa na timu yake ya zamani Azam FC

Azam Fc inadaiwa kuwashawishi Aishi Manula, Erasto Nyoni, John Bocco na Shomaria Kapombe wasaini kunako klabu hiyo waliyokuwa wakicheza kabla ya kusajiliwa na Simba mwaka juzi

Msimu uliopita Bocco aliibuka kuwa mchezaji bora wa Simba na msimu huu ameteuliwa kuwania tuzo hiyo sambamba na Meddie Kagere na Clatous Chama

Zoezi la kuchagua mchezaji bora wa msimu huu tayari limeanza, kura zinapigwa kupitia tovuti rasmi ya Mo Simba Awards

Bonyeza HAPA kumpigia kura Bocco kama unadhani anastahili kuwa mchezaji bora wa Simba msimu huu

Leave a comment