Tetesi za usajili Simba leo 21 May 2019
Kikosi cha Simba leo huenda kikatangaza ubingwa kikicheza kwenye ardhi ya Singida katika uwanja wa Namfua, Simba inahitaji walau sare tu ili kuweza kutangaza Ubingwa mbele ya Singida United wanaohitaji ushindi ili kujihakikishia kuendelea kusalia ligi kuu.
Ukiachana na hayo ya Simba kushinda inaelezwa kuwa kikosi cha Simba kinaendelea kutafuta wachezaji wakuimarisha kikosi chao kwaajili ya msimu ujao.
Kama ulijisahaulisha, mchezaji Vitalis Mayanga wa Ndanda inaelezwa kuwa ni suala la muda tu kutua Simba kwani Simba na Ndanda walishamalizana muda tu na kijana anasubiri ligi iishe waweze kumjumuisha kikosini.
Vitalis Mayanga licha ya kuwa akitajwa kuwaniwa na baadhi ya vilabu nchini Tanzania Yanga ikitajwa lakini imebainika ni mchezaji halali wa Simba anayesubiria ligi iishe aungane na mabingwa hao wa soka nchini.
Credit: Kwataunit