AJIBU Kutimkia TP MAZEMBE

TP Mazembe itamsajili kiungo wa Yanga Ibrahim Ajib Migomba akitarajiwa kujiunga na timu hiyo Julai 01 2019

TP Mazembe imeiandikia barua Yanga kuitaarifu juu ya nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo.

Mazembe itamsajili Ajib baada ya kumaliza mkataba na Yanga

Aidha TP Mazembe imeiomba Yanga impe ruhusa ya siku tatu wiki hii ili aweze kwenda Congo kukamilisha taratibu za usajili

Hii ni habari njema kwa Ajib ambaye msimu huu umekuwa mzuri sana kwake

Ajib ameifungia Yanga mabao sita na kutengeneza mabao 17 kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara inayoelekea ukingoni

Leave a comment