Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura amesema Simba imetawazwa rasmi kuwa mabingwa wa Ligi Kuu baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida Uinted
Ushindi huo uliiwezesha Simba kufikisha alama 91, alama ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine
Wambura amesema Simba walikuwa na timu imara, walionekana kudhamiria kutwaa ubingwa huo tangu mwanzoni mwa msimu
Simba itakabidhiwa kombe keshokutwa Jumamosi, baada ya mchezo dhidi ya Biashara United utakaofanyika uwanja wa Uhuru