AUSSEMS: Ataja sababu ya kubadili kikosi kizima mechi ya Sevilla

Jana Simba nusura iondoke na ushindi wa kihistoria dhidi ya Sevilla katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki uliopigwa uwanja wa Taifa ukimalizika kwa Sevilla kushinda mabao 5-4

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems alifanya mabadiliko ya wachezaji tisa kwenye kipindi cha pili, mabadiliko yanayotajwa kupunguza kasi ya Simba na kupoteza uongozi wa mchezo huo baada ya kuruhusu mabao matatu ndani ya dakika 10

Kocha Mkuu wa mabingwa hao wa Tanzania Bara Patrick Aussems ametetea uamuzi wake akisema ilikuwa muhimu kwa kila mchezaji kupata nafasi kwani ulikuwa ni mchezo wa kihistoria kwa wachezaji wa Simba

“Nilitaka kila mchezaji acheze dhidi ya timu bora kama ya Sevilla,” Aussems aliwaambia waandishi wa habari

“Niliona ni fursa ya kila mchezaji kuweza kucheza mchezo huu dhidi ya Sevilla ili kuweza kupata Uzoefu zaidi ndio maana niliwapa nafasi wachezaji karibia wote kucheza mechi hii kubwa na ya kihistoria dhid ya klabu bingwa mara tano ligi ya Europa”

Simba iliongoza mchezo huo kwa muda mrefu lakini ikapoteza mchezo mwishoni

Mabao ya Simba yalifungwa na John Bocco (2) aliyeibuka nyota wa mchezo, Meddie Kagere na Clatous Chama

Leave a comment