Beki Zana Coulibaly ameshindwa kufikia matarajio ya wengi licha ya kupewa muda wa kutosha kuonyesha makali yake
Beki huyo raia wa Burkina Fasa amepoteza kujiamini, akicheza chini ya kiwango katika michezo ya hivi karibuni
Jana katika mchezo dhidi ya Sevilla, Coulibaly alikumbana na wakati mgumu kutoka kwa baadhi ya mashabiki waliokuwa wakimzomea mara kwa mara kila alipogusa mpira
Kocha Patrick Aussems alimfanyia mabadiliko kwenye kipindi cha pili na nafasi yake kuchukuliwa na Nicholas Gyan
Zana alisajiliwa Simba akiwa na matarajio ya kuziba pengo la Shomari Kapombe ambaye bado yuko nje tangu mwishoni mwa mwaka jana alipopata majeraha wakati akiitumikia timu ya Taifa
Beki huyo huenda akawa miongoni mwa wachezaji watakoachwa katika kikosi cha Simba