SIMBA vs BIASHARA UNITED TAIFA

Mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Biashara United utakaopigwa kesho Jumamosi, May 25, umehamishiwa uwanja wa Taifa na utaanza saa tisa Alasiri

Mabadiliko hayo yatatoa nafasi kwa Simba kukabidhiwa ubingwa baada mchezo huo kumalizika

Uongozi wa Simba umethibitisha mabadiliko hayo na kuwataka mashabiki wa timu hiyo wajitokeze kwa wingi kesho uwanja wa Taifa kupokea ubingwa wa ligi kuu

“Mchezo wa Ligi Kuu ambao tutacheza kesho dhidi ya Biashara United utachezwa katika Uwanja wa Taifa kuanzia saa 9:00 alasiri. Sababu ya mabadiliko ya muda ni sherehe za kukabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu 2018/2019 ambazo zitafanyika baada ya mechi kuisha,” imesema taarifa ya Simba

Leave a comment