Thanks for joining me!
Good company in a journey makes the way seem shorter. — Izaak Walton

Thanks for joining me!
Good company in a journey makes the way seem shorter. — Izaak Walton



Robert Kidiaba Muteba aliyekua mchezaji wa TP Mazembe. Ameteuliwa kuwa Waziri wa michezo wa DRC Congo. Kidiaba alishinda ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.
Full Time



Full Time.
Arsenal 2-0 Newcastle
(Ramsey ⚽ Lacazette ⚽)
#sokaonline

Yanga ilitangulia kupata bao la kuongoza kwenye dakika ya 39 likiwekwa kambani na Heritier Makambo kwa kombora la nje ya 18
Alliance Fc iliyokuwa kwenye kiwango bora ilisawazisha bao hilo kwenye dakika ya 62 kupitia kwa Joseph James
Baada ya kumalizika kwa dakika 90 huku matokeo yakiwa 1-1, changamoto ya mikwaju ya penati ikatumika kuamua mshindi
Deus Kaseke, Paulo Godfrey, Thabani Kamusoko na Haruna Moshi ndio waliofunga penati za Yanga wakati Kelvin Yondani na Mrisho Ngasa walikosa
Yanga sasa itachuana na Lipuli Fc kwenye mchezo wa nusu fainali
MSHAMBULIAJI wa timu ya Taifa yaya Brazil Gabriel Jesus, juzi, aliifungia timu yake mabao mawili ilipopata ushindi wa 3-1 dhidi ya Jamhuri ya Czech.
Brazil walipata ushindi huo kwenye mchezo muhimu wa kirafi ki ambao Brazil walionyesha kiwango cha hali ya juu sana uwanjani.
Wakati Jesus akifunga mabao hayo staa mwingine wa timu hiyo anayeichezea klabu ya Liverpool, Roberto Firmino, alifanikiwa kuifungia timu yake bao lingine moja.
Czech walianza kwa kishindo mchezo huo baada ya kuanza kwa kuongoza kwa bao lililofungwa na David Pavelka katika dakika ya 37 ya mchezo huo.
Kiungo wa Liverpool, Roberto Firmino aliisawazishia timu yake mapema kipindi cha pili, kabla Jesus hajafunga mabao mawili kipindi cha pili cha mchezo huo.
Brazil wamerejea kwenye ushindi baada ya wikiendi iliyopita kupata sare ya bao 1-1 na Panama.
Mastaa wa Brazil, Firmino, Philippe Coutinho na kipa wa Liverpool, Alisson walionyesha kiwango cha juu sana kwenye mchezo huo.

Mabao ya Simba yalipatikana kwenye kipindi cha pili yakiwekwa kambani na beki Paul Bukaba (51′) huku bao la pili likifungwa na Meddie Kagere kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 55 baada ya Adam Salamba kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems alifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake leo akiwapumzisha baadhi ya nyota waliocheza mchezo wa ligi ya mabingwa mwishoni mwa wiki
Aidha bao alilofunga Kagere leo limemfanya afikishe mabao 13 sasa akishika nafasi ya pili nyuma ya Salim Aiyee wa Mwadui Fc mwenye mabao 16
Simba inaendelea kushika nafasi ya tatu ikiwa imefikisha alama 54, alama tano nyuma ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili huku Yanga ikiongoza ikiwa na alama 67
Hata hivyo Azam Fc na Yanga zimecheza michezo saba zaidi ya Simba