Stars yawekwa chungu cha nne, upangaji makundi AFCON 2019

Droo ya makundi ya michuano ya AFCON 2019 inafanyika leo saa tatu usiku huko Misri ambapo Tanzania iliyofuzu baada ya kusubiri miaka 39, itakuwa miongoni mwa timu 24 zitakazoshiriki michuano hiyo mwaka huu

Katika droo hiyo, timu zitapangwa kwenye makundi sita ya timu nne nne

Droo ya makundi itafanyika kwa kuchagua timu kutoka kila chungu miongoni mwa vyungu vinne vyenye timu sita sita ambazo zimewekwa kwa kufuata ubora

Tanzania imewekwa kwenye chungu cha nne sambamba na Namibia, Guinea Bissau, Angola, Burundi na Zimbabwe

Timu zinazokuwa kwenye chungu kimoja haziwezi kupangwa kundi moja hivyo Stars haiwezi kupangwa na timu zilizotajwa hapo juu