



Kikosi cha Simba Sc vs Js Saoura #CCL


Makamanda wetu wakipata chakula cha mchana. Burudani inaendelezwa baadae tutakapocheza na JS Saoura. #NguvuMoja


Muonekano wa uwanja mpya wa Tottenham Hotspurs



Ratiba ya mechi za leo Tpl
Miongoni mwa wachezaji waliojumuishwa katika kikosi hicho, Aishi Manula, Jonas Mkude na John Bocco wametoka katika klabu ya Simba


Taarifa iliyotufikia muda huu ni kwamba Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde amefariki dunia leo Machi 7, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amethibitisha kwamba Kibonde amefariki akiwa Mwanza, alianza kusumbuliwa na Presha toka Bukoba kwenye msiba wa Ruge Mutahaba na kuhamishiwa Mwanza.

Aidha, siku chache zilizopita, Clouds Media iliondokewa na mkurugenzi wake wa vipindi, Ruge Mutahaba aliyezikwa nyumbani kwao wilayani Bukoba mkoa wa Kagera.
Soka Updates inatoa pole kwa CLOUDS MEDIA GROUP.
Kocha Mkuu wa Stars Emmanuel Amunike kesho Ijumaa March 08 anatarajiwa kutangaza kikosi cha Stars

Mchezaji MBWANA SAMMATA Ameingia kwenye Top 5 ya waliofunga magoli mengi Kwenye Michuano Yote


Credit: #Sokaonline
Mshambuliaji wa timu ya Simba, Meddie Kagere amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Februari wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) msimu wa 2018/2019.

Kagere raia wa Rwanda ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wenzake wawili, Salim Aiyee wa Mwadui na Salum Kimenya wa Prisons alioingia nao fainali.

Kamati ya Tuzo pia imemchagua Kocha wa Prisons ya Mbeya, Mohamed Rishard kuwa Kocha Bora wa mwezi Februari akiwashinda Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems na Kocha Mkuu wa Mwadui, Ally Bizimungu.