Taarifa kuhusu mechi ya Simba vs JKT Tanzania

Taarifa kuhusu mechi ya Simba vs JKT Tanzania
Mechi kati ya Simba dhidi ya JKT Tanzania iliyopangwa kuchezwa leo katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro huenda isichezwe kutokana na hali ya mvua kubwa kunyesha na uwanja kujaa maji.

Kwasasa kinachosubiriwa ni nusu saa kupita kulingana na kanuni za kuahirisha mechi, ambayo kanuni mojawapo inataka angalau ipite nusu saa ndipo mechi ihairishwe.