Shirikisho la soka nchini (TFF) limeweka hadharani Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinachotarajia kucheza mchezo wa kufuzu AFCON dhidi ya Lesotho Novemba 18,2018 Mjini Maseru,Lesotho.
Kiungo wa Simba Shiza Kichuya amerejeshwa katika kikosi hicho na kocha Emmanuel Amunike baada ya kukosa mchezo uliopita
Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Jonas Mkude na John Bocco pia wameitwa.
