LIGI: Ya mabingwa AFRICA kuanza mwezi huu

Mchezo wa fainali wa michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa msimu uliopita utapigwa kesho Ijumaa kati ya Al Ahly dhidi ya Esperance.

Kufuatia mabadiliko ya kalenda ya michuano hiyo yaliyofanywa na CAF, Novemba 28 michezo ya hatua ya awali ya michuano hiyo kwa ajili ya msimu huu inaanza

Ratiba ya michezo ya awali inatarajiwa kupangwa wiki ijayo jiji la Cairo nchini Misri.

Simba, mabingwa wa soka Tanzania Bara ndio wawakilishi wa nchi kwenye michuano hiyo msimu huu.

Wanatarajiwa kuanza kampeni yao kati ya tarehe 27 na 28 mwezi huu wakisubiri kumfahamu mpinzani wao wiki ijayo.

Michezo ya marudiano kwa hatua ya awali itapigwa baada ya wiki moja

Timu zitakazofuzu hatua ya awali zitatinga raundi ya kwanza na kama zitashinda kwenye hatua hiyo zitafuzu kwa hatua ya makundi.

Kwa zile zitakazotolewa kwenye raundi ya kwanza zitahamishiwa kwenye raundi ya pili ya michuano ya kombe la Shirikisho

Kuanzia msimu huu michuano hiyo itakuwa inamalizika mwishoni mwa mwezi wa tano.

Leave a comment