NIYONZIMA: Atoswa Timu Ya Taifa RWANDA

Kiungo wa Simba Haruna Niyonzima hajajumuishwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Rwanda kinachojiandaa na mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON 2019 dhidi ya Afrika ya Kati.

Mchezo huo utapigwa nchini Rwanda Novemba 18.

Niyonzima amekuwa kwenye mgogoro na uongozi wa Simba uliopelekea afanye migomo ya mara kwa mara na hivyo kuondolewa kwenye kikosi cha kwanza cha mabingwa hao wa Tanzania Bara.

Wakati Niyonzima akiondolewa kwenye kikosi hicho cha Rwanda, Meddie Kagere kinara wa mabao kwenye kikosi cha Simba ameitwa.

Idadi kubwa ya wachezaji wa Simba wameitwa kwenye timu za mataifa yao kwa ajili ya michuano ya AFCON.

Emmanuel Okwi na Juuko Murshidi wao wameitwa timu ya Taifa ya Uganda, wakati Cleotus Chama ‘CCC’ yeye ameitwa timu ya Taifa ya Zambia.

Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Shiza Kichuya na John Bocco wao wameitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inayotarajiwa kusafiri leo kwenda kuweka kambi nchini Afrika Kusini.

Leave a comment