Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba Ijumaa, Novemba 16 2018 watashuka kwenye uwanja wa Taifa kuikabili Big Bullets kutoka Malawi katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki.
Mchezo huo utapigwa kuanzia saa 12 jioni na utarushwa mbashara na Azam Sport 2.
Mchezo huo uliombwa na kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems ili kukipima kikosi chake ambacho mwishoni mwa mwezi huu kitacheza mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa dhidi ya Mbabane Swallows.
Hata hivyo katika mchezo huo Simba itawakosa wachezaji wake 12 walioitwa kwenye vikosi vya timu za Taifa