Afisa Habari wa Simba Haji Manara amemshukia mwandishi na mchambuzi wa soka nchini Shaffih Dauda baada ya kuweka taarifa kwenye ukurasa wake wa matandao kijamii kuwa kiungo Haruna Niyonzima yuko mbioni kusajiliwa na Azam Fc.
Manara ameshangazwa na taarifa hizo alizodai ni za kiuchonganishi.
“Tunajua Shaffih unatumika na Maadui wa Simba kutaka kutuvuruga kusudi ili kubalance na sisi tuonekane tuna mgogoro na wachezaji wetu,” ameandika Manara.
“Haruna Niyonzima yupo kambini na leo atacheza ikimpendeza kocha dhidhi ya Bata Bullets.
“Hivi mtu muungwana kabisa unawezaje kuandika uongo na kufikia kumvalisha jezi ya timu nyingine mchezaji aliye na mkataba na klabu yetu kama si uchochezi na uhuni wa kishamba?,” amehojia Manara