USAJILI: Yanga kushusha Kifaa Hiki Kutoka UGANDA

Taarifa za uhakika ni kwamba Yanga imekamilisha mazungumzo na mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda Nelson Senkatuka anayechezea Bright Stars inayoshiriki ligi kuu nchini humo.

Senkatuka anatarajiwa kutua nchini wiki ijayo ili kukamilisha taratibu za usajili tayari kuanza kuwatumikia mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania.

Msimu uliopita Senkatuka aliifungia Brights Stars mabao 18 kwenye ligi kuu ya Uganda.

Mabosi wa Kamati ya usajili ya Yanga wako ‘busy’ kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili kuhakikisha wanaongeza nguvu kwenye kikosi cha timu hiyo ambacho kinashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi