KAIZER CHIEF YAMNYEMELEA OKWII

Wachezaji waandamizi wa kikosi cha Simba wameanza kunyemelewa kwa kasi na timu vigogo barani Afrika kutokana na kiwango kikubwa wanachoonyesha sasa.

Baada ya klabu za AS Vital na Zamalek kujitosa kumuwania Meddie Kagere, Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini nayo imejitosa kumuwania Emmanuel Okwi kulingana na Mwanaspoti

Chiefs ambayo iko visiwani Zanzibar kurudiana na Zimamoto kwenye mchezo wa kombe la Shirikisho, inadaiwa kutuma ofa ikitaka kumsajili kinara huyo wa mabao wa kikosi cha Simba

Okwi alirejea Simba msimu uliopita na katika msimu wake wa kwanza alifanikiwa kuwa mfungaji bora baada ya kufunga mabao 20.

Msimu huu tayari ameifungia Simba mabao saba akiwa nyuma ya Eliudi Ambokile wa Mbeya City anayeongoza na mabao tisa.

Uongozi wa Simba utakazimikia kufanya kazi ya ziada kuhakikisha washambuliaji wake hawachukuliwi na timu nyingine

Kwani ili kuweza kufikia malengo ya kuifanya Simba kuwa bingwa wa Afrika inahitaji kuwa na wachezaji hawa ambao tayari wameonyesha uwezo usio na shaka