
Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Yanga jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa timu hiyo Dk Mshindo Msolla amesema tayari uteuzi umeshafanyika kwa sasa wanafanya majadiliano na wajumbe walioteuliwa kabla ya kuwaweka hadharani
“Wajumbe wa Kamati hiyo tumeshawateua lakini hatuwezi kuwatangaza kabla nao hawajaridhia,” amesema Dk Msolla
“Wiki ijayo tutakuwa na kikao na benchi la Ufundi, pengine katika kikao hicho tutaitangaza Kamati”
“Msimu huu tumedhamiria kufanya usajili makini wenye tija”
Aidha Dk Msolla amesema hata hivyo jukumu la kutafuta wachezaji litabaki kwa kocha Zahera na benchi lake la ufundi, Kamati hiyo itakuwa na jukumu la kumsaidia kukamilisha michakato ya usajili baada ya makubaliano kufikiwa
Dk Msolla amesema kuanzia msimu ujao watawatumia wachezaji waliocheza Yanga zamani kutafuta wachezaji
“Msimu ujao kazi kubwa itafanywa na wachezaji wetu wa zamani kwani tutawapa jukumu la kutembea mikoani kutafuta wachezaji wenye vipaji”