Wakati akisajiliwa na Simba mwaka jana, wapo waliobeza usajili wa Meddie Kagere wakidai Simba haitanufaika na usajili wake kwa kuwa umri tayari umemtupa mkono
Hata hvyo mpaka sasa msimu unapoelekea ukingoni, hakuna hata mmoja atajitokeza kumbeza Kagere kutokana na alichokifanya katika klabu ya Simba ndani ya mwaka mmoja
Kagere ndiye kinara wa mabao kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara, jana akiitungua Ndanda Fc mabao mawili yaliyomfanya afikishe mabao 22
Kwa michezo iliyobaki, ni dhahiri Kagere ataibuka mfungaji bora wa ligi kuu ya Tanzania Bara kwani mabao yake 22 yanamfanya aongoze kwa tofauti ya mabao sita dhidi ya wanaomfuatia, Salim Aiyee na Heritier Makambo ambaye tayari ameondoka Yanga
Kagere ameichezea Simba michezo 50 katika mashindano yote
Amefunga mabao 33 na kutoa pasi nne za mabao
Ana wastani wa kufunga zaidi ya bao moja kila mchezo
Kagere alitoa mchango mkubwa kwa kikosi cha Simba kwenye michuano ya ligi ya mabingwa msimu huu, akifunga mabao sita
Kwa kushirikiana na washambuliaji wengine, John Bocco na Emmanuel Okwi, wameifanya Simba iwe moto wa kuotea mbali katika kuzifumania nyavu kwenye ligi
Watatu hao pekee wamefunga mabao 52 kati ya mabao 74 yaliyofungwa na Simba