ZAHERA: amefichua kuwa aliwasiliana na viongozi wa TP Mazembe wiki tatu zilizopita kuhusu usajili wa kiungo Ibrahim Ajib

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amefichua kuwa aliwasiliana na viongozi wa TP Mazembe wiki tatu zilizopita kuhusu usajili wa kiungo Ibrahim Ajib

Zahera amesema kwa uwezo alioonyesha kwenye kikosi cha Yanga, Ajib anaweza kufanikiwa kukipiga TP Mazembe lakini ni lazima abadilike

“Nilisimulia na TP Mazembe wiki tatu zilizopita juu ya Ajib,” amesema Zahera

“Sina wasiwasi na yeye kusajiliwa TP Mazembe sababu nafahamu ni mchezaji mzuri sana”

“Lakini inafaa akajitume sana ili kuweza kupata namba TP Mazembe”

“Mpira wa TP Mazembe ni mpira wa nguvu mingi, yafaa akatumike sana ili aweze kucheza”

Leave a comment