Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema wachezaji wa kigeni wanaotarajiwa kusajiliwa na timu hiyo wote wanacheza katika timu zao za Taifa
Zahera amesema usajili wa wachezaji wa kigeni umezingatia umuhimu wa kusajili wachezaji ambao wataongeza ushindani na kuinua kiwango cha wachezaji wa ndani
“Miongoni mwa wachezaji tutakaowasajili, sita au saba ni wachezaji wa kigeni. Wageni wote wanaokuja Yanga wanacheza timu za Taifa. Watasaidia kuongeza ushindani wa kikosi chetu na kuinua viwango vya wachezaji wazawa,” amesema
Kuhusu usajili wa wachezaji wa ndani, Zahera amesema hawatafanya usajili mkubwa wa wachezaji wa ndani
“Nafikiri tutasajili wachezaji watatu au wanne wa ndani. Tunao wachezaji wazuri ambao tutawaimarisha ili msimu ujao wawe bora zaidi”
Kuhusu wachezaji wanaoachwa, Zahera amesema wataachana na wachezaji 10 ambao majina yao yatafahamika baada ya kumalizika kwa mchezo wa mwisho wa ligi dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Jumanne, May 28 2019