Kiungo fundi Haruna Niyonzima amekuwa kwenye kiwango bora sana. Tangu kuanza kwa mwaka 2019, Niyonzima amekuwa mchezaji wa kutegemewa wa kikosi cha Simba kinachonolewa na Mbelgiji Patraick Aussems
Niyonzima ni miongoni mwa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika na tayari mazungumzo ya kumuongezea mkataba yameanza
Akiwa miongoni mwa wachezaji walioisaidia Simba kutwaa ubingwa wa pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara, hakuna shaka, ataendelea kubaki Msimbazi
Kiungo huyo wa zamani wa APR, amekiri juu ya kuanza kwa mazungumzo ya mkataba mpya
“Kwa sasa hivi siwezi kuweka kila kitu wazi, muda utakapofika taarifa zitawekwa hadharani, ngoja tumalizie msimu huu kwanza,” alisema Niyonzima
Juzi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ alisema Bodi hiyo ilikuwa ikisubiri ripoti ya kocha Patrick Aussems ili kuanza michakato ya usajili
Inaelezwa tayari Aussems ameshawasilisha ripoti hiyo