
– Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania, Adi Yussuf Rasmi Amethibitisha kuachana na Klabu aliyokuwa akiichezea, Solihull Moors FC ya National League nchini Uingereza (Daraja La tano) Baada ya kutofikia muhafaka wa Mkataba mpya kwa ajili ya msimu ujao.
.
– Adi mwenye umri wa miaka 26, Alijiunga na klabu hiyo January 25,2018 kwa Mkataba wa mwaka Mmoja na Nusu Baada ya kumaliza Mkataba wake na Klabu ya Barrow nayo ya National League akiichezea mwaka mmoja tu tangu ajiunge nao Julai 29, 2017.
.
– Katika Game yake ya kwanza tu akiwa na Solihull alifunga Magoli mawili katika Dakika mbili dhidi ya Dagenham akicheza Dakika 70.. Tangu hapo kacheza game zaidi ya 50 na kufunga Magoli zaidi ya 20..@adiyussuf anajiandaa kutua Nchini tayari kujiunga na kambi ya @taifastars_ kujiandaa na Maandalizi ya AFCON 2019.
#Tanzania #TotalAFCON2019
@Sokawaytz
credit: @sokawaytz
