#TetesiZaUsajili Imeripotiwa kuwa klabu ya Simba Sc ipo kwenye mchakato mzito kuhakikisha inamsajili nyota wa zamani wa Tp Mazembe Thomas Ulimwengu (25) kuelekea kwenye dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa mapema wiki ijayo November 15.
Habari za chini chini zilizotufikia zimedai tayari uongozi wa klabu hiyo umepanga mkakati wa kuanza kuzungumza nae wiki hii ili kupata saini yake mara baada ya kuvunja mkataba na klabu yake ya Al Hilal ya Sudan
Ikumbukwe kabla ya kutua Al Hilal ziliwahi kuzagaa taarifa kuwa nyota huyo angesajiliwa Yanga kutokana na uongozi wa klabu hiyo kuonyesha nia ya kumhitaji #soka Updates