SIMBA : Baada ta BOCCO : OKWI MKUDE

Simba tayari imeanza mchakato wa kuhuisha mikataba ya wachezaji wake ambayo inamalizika mwishoni mwa msimu

Baada ya kumalizana na nahodha John Bocco, inaelezwa mshambuliaji Emmanuel Okwi na Jonas Mkude wako katika mazungumzo na uongozi wa Simba ili kuhuisha mikataba yao

Wachezaji hao wanadaiwa kunyemelewa na timu nyingine hivyo kuulazimu uongozi wa Simba kuharakisha kuwapa mikataba mipya

Okwi amekuwa akihusishwa na timu kadhaa kutoka Afrika Kusini, ambapo mwezi Januari Kaizer Chiefs iliwasilisha ofa kwa klabu ya Simba lakini uongozi ‘ukaipiga chini’

Mkude anatajwa kuwaniwa na timu kadhaa kutoka Arabuni

Wachezaji wengine ambao wako katika mipango ya mwalimu na watasaini mikataba mipya pia

Aidha Simba huenda isifanye mabadiliko makubwa ya kikosi chake hasa kwa wachezaji wa ndani baada ya Aussems kuagiza waliopo waongezewe mikataba kwa kuwa nje ya Simba hakuna wachezaji wengi bora

Wachezaji wa ndani wanaotajwa kujiunga na Simba kwa ajili ya msimu ujao ni pamoja na Vitalis Mayanga kutoka Ndanda Fc.

Mayanga alisajiliwa kwa ajili ya michuano ya CAF lakini taarifa zake zikachelewa kutumwa

Wengine ni Ibrahim Ajib kutoka Yanga na Beno Kakolanya (huru)

Leave a comment