KRC GENK anayochezea mtanzania Mbwana Samatta imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi kuu nchini Ubelgiji

Klabu ya KRC GENK anayochezea mtanzania Mbwana Samatta imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi kuu nchini Ubelgiji maarufu kama Belgium Pro League mara baada ya kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Anderlecht huku ikisaliwa na mchezo mmoja mkononi.
.
Genk itamaliza mchezo wake wa mwisho ikiwa nyumbani dhidi ya St.Liege.
.
.
Hongera @samagoal77

Esperance yatinga fainali ligi ya mabingwa, kucheza na Wydad Casablanca

Esperance imetinga fainali ligi ya mabingwa Barani Afrika baada ya kuiondosha TP Mazembe kwa ushindi wa bao 1-0

Esperance leo imeilazimisha TP Mazembe suluhu ya bila kufungana katika mchezo uliopigwa dimba la Mazembe, Lubumbashi huku ikitoka kushinda bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza

Mamelodi Sundowns pia imeshindwa kupindua matokeo ya 2-1 iliyofungwa na Wydad Casablanca kwenye mchezo wa kwanza baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana

Esperance imetinga fainali kwa msimu wa pili mfululizo sasa itachuana na Wydad Casablanca michezo miwili ya fainali itakayopigwa mwishoni mwa mwsi huu

Mchazaji Neymar Afungiwa Mechi 3 Kutokana na Alichoandika Instagram

Shirikisho la Soka Barani Ulaya(UEFA) limemfungia mshambuliaji huyo wa Paris Saint-Germain baada ya kuandika maneno ya dharau na kejeli kufuatia timu yake kutolewa na Manchester United katika mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya

Mbrazili huyo, aliweka bandiko katika ukurasa wake wa mtandao wa Kijamii wa Instagram lenye kuonesha hasira baada ya Man. Utd kupata penati ndani ya dakika nne za nyongeza wakati shuti lililopigwa na Diogo Dalot lilipomgonga Presnel Kimpembe mkononi

-l

Marcus Rashford alitumia nafasi hiyo aliyopewa na Muamuzi Damir Skomina aliyetoa penati hiyo baada ya kujishauri kutumia mfumo wa uamuzi wa runinga(VAR), kufunga goli na kufanya Manchester United kufuzu kucheza hatua ya robo fainali

Neyma aliandika “Hii ni aibu, wameweka watu wanne wasiojua chochote kuhusu soka kutoa maamuzi baada ya kuangalia marudio ya tukio kupitia VAR. Hakukua na penati. Panawezaje kuwa na penati wakati mpira umempiga mgogoni!” Kisha akatuna

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO JUMATATU

Kiwango cha mshahara anachokitaka kiungo wa Manchester United Paul Pogba, 26, kinaweza kikawa kikwazo kwa Real Madrid kumsajili nyota huyo raia wa Ufaransa. (AS)

Chelsea wannapiga hesabu za kumnyakua kiungo wa Brazil na klabu ya Barcelona Philippe Coutinho, 26, kama mbadala wa mshambuliaji wao raia wa Ubelgiji Eden Hazard, 28, ambaye mwisho wa msimu anatarajiwa kuhamia Real Madrid.(Calciomercato)
Klabu ya Manchester United ipo tayari kumpandisha Mike Phelan mpaka kuwa mkurugenzi wa ufundi, na nafasi yake ya meneja msaidizi kupewa kiongo wa zamani wa klabu hiyo Michael Carrick. (Mail)

Mchezaji nyota wa zamani wa Arsenal ambaye pia alitimuliwa kwenye kazi ya ukufunzi na klabu ya Monaco, Thierry Henry, 41, yumo kwenye mazungumzo na klabu ya New York Red Bulls ya ligi ya soka Marekani ili kujiunga nao kama mkufunzi. (Sky Sports)
Mshambuliaji nyota wa Ufaransa na klabu ya PSG Kylian Mbappe, 20, amekanusha uvumi ulioenea kuwa ana mpago wa kuhamia Real Madrid. Mbappe ametoa kauli hiyo baada ya kuifunga goli tatu timu yake ya zamani Monaco. (Goal.com)
Beki raia wa Brazil Marcelo, amesisitiza kuwa hana mpango wa kuihama klabu yake ya Real Madrid mwishoni mwa msimu – licha ya uvumi kuenea kuwa mchezaji huyo alikuwa akitammani kuungana tena na Cristiano Ronaldo, katika klabu ya Juventus. (Bein Sports, via Mirror)

Marcelo
Image captionMarcelo (kulia) ameamua kuuzima uvumi kuwa anajipanga kuhamia Juventus mwishon mwa msimu.
Kocha wa muda mrefu wa wachezaji chipukizi wa Aston Villa Sean Kimberley ameikacha klabu hiyo. (Birmingham Mail)
Bosi wa Newcastle Rafa Benitez amedai kuwa mfumo wa mishahara wa klabu hiyo unaifanya timu isiwe na matokeo mazuri kwenye Ligi ya Premia. (Newcastle Chronicle)
Rafa Benitez
Image captionRafa Benitez amekuwa akihusishwa na mipango ya kuihama Newcastle
Mshambuliaji wa Newcastle raia wa Uhispania Ayoze Perez, 25, ameashiria kuwa anataka kuihama klabu hiyo mwushoni mwa msimu. (Mirror)

Rais wa klabu ya Nice ya Ufaransa Gauthier Ganaye amesema klabu yake huenda ikamsajili mshambuliaji wa Chelsea Olivier Giroud, 32. (Goal.com