TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO JUMATATU

Streka wa PSG na Ufaransa Kylian Mbappe, 20, amebainisha kuwa anaweza kuihama klabu yake katika kipindi hiki cha usajili. Kauli hiyo inatarajiwa kuziamsha klabu kongwe na tajiri kama Real Madrid, Barcelona na Manchester City kumgombea. (Express)

Kiungo raia wa Ujerumani Ilkay Gundogan, 28, anataka kurudi mezani na klabu yake ya Manchester City kwa malengo ya kusalia klabuni hapo zaidi ya mwezi Juni 2020 ambapo mkataba wake wa sasa unaishia. (Mail)
Kocha Pep Guardiola atapewa fursa ya kusalia klabuni Manchester City walau kwa miaka mitano ijayo huku kipato chake kikifikia pauni milioni 100, baada ya mshahara wake kwa mwaka kuchupa toka pauni milioni 15 mpaka milioni 20. (Sun)

Kiungo wa kimataifa wa Ubelgiji Yannick Carrasco, 25, ambaye anakipiga kwenye ligi kuu ya Uchina, klabu ya Dalian Yifang, anataka kuhamia katika ligi ya Primia na Arsenal wanatarajiwa kumnyemelea, klabu hiyo ilikaribia kumsajili katika dirisha dogo la usajili la Januari. (Sun)

Arsenal pia wanamnyemelea beki wa kati na kinda wa timu ya Saint-Etienne na timu ya taifa ya chini ya miaka 19 ya Ufaransa, William Saliba, 18. (Goal.com)

SanchezHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Sanchez amekuwa na wakati mgumu na United tofauti na alipokuwa Arsenal
Mshambuliaji aliyepoteza kiwango wa Manchester United na Chile Alexis Sanchez, 30, anatarajiwa kukatiza mapumziko yake ya mwisho wa msimu na kurudi klabuni ili kujifua na kujihakikishia nafasi katika kikosi cha United. (Sun)
Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amemwonesha dalili za wazi winga raia wa Wales Gareth Bale, 29, kuwa muda wake katika klabu hiyo umefikia tamati, baada ya kusema kuwa asingemuingiza mchezoni kutoka benchi walipofungwa Jumapili na Real Betis hata kama kungekuwa na fursa ya kuingiza wachezaji wanne. (Eurosport)
BaleHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption Bale ‘agoma’ kuhama Real Madrid mpaka mkataba wake utakapoisha
Bale hata hivyo amewaambia wachezaji wenzake kuwa anapanga kusalia klabuni hapo mpaka kwisha kwa mkataba wake na takuwa mwenye furaha kucheza gofu endapo hatapangwa kucheza. (Radioestadio, via Mail)

Kiungo wa Chelsea na Ufaransa N’Golo Kante, 28, anapiga hessabu za kuikacha klabu yake na kujiunga na miamba ya Ligi ya Ufaransa PSG. (Talksport)
KanteHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Manchester United watarasimisha nia yao ya kumsajili kiungo wa Lyon, Tanguy Ndombele, 22, pale tu mustakabali wa kiungo wao Paul Pogba, 26, utakapokuwa wazi. (Manchester Evening News)

Kocha wa Lille, Christophe Galtier amethibitisha kuwa winga raia wa Ivory Coast winger Nicolas Pepe, 23, ataihama klabu hiyo hivi karibuni. Mcezaji huyo anahusishwa na uhamisho na klabu kongwe za Manchester United, Arsenal na Bayern Munich. (Manchester Evening News)

Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu nchini Italia “Serie A” kwa msimu 2018/19

✍🏼 Mshambuliaji wa Klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu nchini Italia “Serie A” kwa msimu 2018/19, Cr7 ametwaa tuzo hii ikiwa ni msimu wake wa kwanza tu kusakata soka nchini Italia.
:
✍🏼 Ronaldo alikuwa sehemu ya kikosi cha Vibibi hivyo vya Turin kwenye kutwaa Scudetto yao ya nane mfululizo huku Cr7 ikiwa ni ya kwanza kwake na yeye mwenyewe akipachika Mabao yake 21 katika Ligi. Tuzo za Serie A kila mshindi anapewa baada ya kumalizika kwa msimu, lakini Ronaldo atapewa tuzo yake kabla ya mchezo wao dhidi ya Atalanta siku ya leo Jumapili.
:
✍🏼 Wachezaji wengine waliotwaa tuzo katika Ligi hiyo ni, Mlinda lango Bora wa Msimu katokea Inter Milan, Samir Handanovic, Beki Bora wa Msimu imebebwa na Muafrika kutoka Senegal, Kalidou Koulibaly anaekipiga Napoli, Kiungo Bora Ligi Kuu Italia imebebwa na fundi wa kumiliki Dimba La Kati, Sergej Milinkovic-Savic kutoka Klabu ya Lazio, Fabio Quagliarella Mshambuliaji hatari wa Sampdoria kabeba tuzo ya Mshambuliaji bora wa msimu na Nicolo Zaniola kinda ambaye anacheza Klabu ya AS Roma, yeye kaibuka Mchezaji bora kijana wa Mwaka ndani ya Serie A.
:
✍🏼 Ronaldo Sasa katwaa tuzo ya Mchezaji bora wa mwaka Italia, England na Hispania pamoja na kutwaa Ubingwa wa Ligi kwa nchi zote tatu.. Koulibaly amekuwa nguzo ya ulinzi ndani ya Napoli blocks 31, Clearance 125, tackles won 60 Kati ya 67, clean sheets 13 katika mechi 31 alizocheza..
#seriea #juventus #napoli #lazio #asroma
@Sokawaytz

SEVILLA – Kuwasili Dar Mei 21

Leo Jumamosi Sevilla inakamilisha mchezo wa mwisho ligi kuu ya Hispania , La Liga kwa kucheza na Athletic Club

Kama itashinda mchezo huo, Sevilla inayoshika nafasi ya sita kwenye msimamo wa La Liga , inaweza kukata tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao

Baada ya mchezo huo, kikosi cha Sevilla itaanza safari ya kuja nchini tayari kwa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa Tanzania Bara, Simba

Sevilla inatarajiwa kuwasili nchini Mei 21 kuelekea mchezo huo utakaopigwa Mei 23, uwanja wa Taifa kuanzia saa moja jioni

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, (TFF) limesema kuwa ujio wa timu ya Sevilla kutoka nchini Hispania chini ya SportPesa Tanzania utaongeza hamasa na maendeleo ya mpira wa miguu nchini.

TFF imewataka wachezaji wa Simba kutumia fursa ya mechi hiyo kuonyesha uwezo na vipaji vyao ili kujitangaza

Rais wa TFF, Wallace Karia amesema kuwa Sevilla FC ni timu kubwa yenye historia kubwa katika soka duniani na hivyo ujio wao utawavutia mashabiki wa soka hata wa nchi jirani ili kuja kushuhudia wachezaji nyota wa wanaocheza bara la Ulaya.

CASILLAS: Mlinda lango wa Kimataifa wa Hispania, Iker Casillas Ametangaza kustaafu Soka rasmi hii leo;

– Mlinda lango wa Kimataifa wa Hispania, Iker Casillas Ametangaza kustaafu Soka rasmi hii leo; hili limekuja siku chache Baada ya kuruhusiwa hospitali ambako alikimbizwa kufuatia kupata Shambulio La Moyo wakati akiwa katika Mazoezi ya Klabu yake ya FC Porto..
.
– Legendary huyo amefanikiwa kucheza jumla ya mechi 881 ngazi ya Vilabu na games 167 katika timu yake ya taifa ya Hispania na makombe aliyotwaa ni Kama..
• 1x World Cup 🏆
• 2x Euro Championship 🏆
• 3x Champions League 🏆 • 5x La Liga 🏆
• 2x Copa del Rey 🏆
• 1x Club World Cup 🏆
• 1x Primeira Liga 🏆
🙌🏽🐐 #Updates

RATIBA YA SOKA HII LEO JUMAMOSI:

RATIBA YA SOKA HII LEO JUMAMOSI:
– Serie A
16:00 Udinese
SPAL
19:00 Genoa
Cagliari
21:30 Sassuolo
Roma
.
– FA Cup FINAL!!
19:00 Manchester City
Watford
.
– Bundesliga
16:30 Bayern München
Eintracht Frankfurt
16:30 Borussia M’gladbach
Borussia Dortmund
16:30 Fortuna Düsseldorf
Hannover 96
16:30 Freiburg
Nürnberg
16:30 Hertha BSC
Bayer Leverkusen
16:30 Mainz 05
Hoffenheim
16:30 Schalke 04
Stuttgart
16:30 Werder Bremen
RB Leipzig
16:30 Wolfsburg
Augsburg
.
– Ligue 1
22:00 Bordeaux
Reims
22:00 Guingamp
Nîmes
22:00 Lille
Angers SCO
22:00 Monaco
Amiens SC
22:00 Montpellier
Nantes
22:00 Olympique Lyonnais
Caen
22:00 PSG
Dijon
22:00 Saint-Étienne
Nice
22:00 Strasbourg
Rennes
22:00 Toulouse
Olympique Marseille
.
– La Liga
14:00 Levante
Atlético Madrid
17:15 Espanyol
Real Sociedad
17:15 Getafe
Villarreal
17:15 Real Valladolid
Valencia
17:15 Sevilla
Athletic Club
21:45 Celta de Vigo
Rayo Vallecano
21:45 Deportivo Alavés
Girona
21:45 Huesca
Leganés
.
– UEFA Women’s Champions League – FINAL!!
19:00 Olympique Lyonnais
Barcelona
.
– Belgium – First Division A.
(EL play-off: group A)
21:00 KFCO Beerschot-Wilrijk
Oostende
21:00 Sporting Charleroi
Eupen
21:00 St.Truiden
Westerlo
.
– Ligi Kuu Bara.
16:00 African Lyon
Mbeya City FC
.
– Kenya – Premier League.
14:00 MT Kenya United
SoNy Sugar
15:00 Kariobangi Sharks
KCB
15:00 Nzoia Sugar FC
Sofapaka
16:15 Posta Rangers
Kakamega Homeboyz
.
– Morocco – Botola Pro
22:00 Difaa El Jadida
Hassania Agadir
22:00 Rapide Club Oued Zem
OCK Khouribga
.
– South Africa – Cup.
20:00 Kaizer Chiefs
TS Galaxy
:
MECHI ZA JANA
– Belgium – First Division A.
(EL play-off: group)
FT Kortrijk 4 – 0 Cercle Brugge
FT Royal Excel Mouscron 2 – 4 Waasland-Beveren
FT Zulte-Waregem 2 – 1 Union St.-Gilloise
#Updates @Sokawaytz

MAN U – Yaanza Mikakati ya Kusuka Kikosi Bora Msimu Ujao

✍🏼 Kujenga kikosi ndani ya Manchester United kumeanza, Miamba hao wa Old Trafford Rasmi imewasiliana na klabu ya Fulham mara moja juu ya kutaka kumsajili kinda wao, Ryan Sessegnon.
:
✍🏼 United itakutana na Upinzani kwani, Tottenham na Juventus pia wanavutiwa na kijana huyo, ambaye leo anatimiza umri wa miaka 19, lakini United ni timu pekee ambayo imetuma maombi yao kuwasiliana na Fulham hadi sasa.. Kwa mujibu wa chanzo makini @skysports.
:
✍🏼 Sessegnon inaeleweka kuwa hawezi kucheza msimu mwingine katika Championship kufuatia Fulham kushuka daraja ikiwa ni msimu mmoja tangu wapande Premier league, United wanataka kuongeza vipaji kwa kusajili wachezaji vijana katika kikosi cha kocha Ole Gunnar Solskjaer..
:
✍🏼 Fulham huenda wakakubali kufanya Biashara ya kumuuza Sessegnon kwa vilabu vinavyomtaka kwani kinda huyo kabakiza Mkataba wa Mwaka mmoja tu kuwatumikia watoto hao wa London..
#transfers #Updates #premierleague
@Sokawaytz