PAUL POGBA

Imeelezwa kuwa Kiungo wa Man United Paul Pogba hana uhusiano mzuri na kocha wake Ole Gunnar Solskjaer huenda sababu hiyo ikarahisisha kiungo huyo kuhamia Real Madrid mwishoni mwa msimu huu (Le Parisien via AS)

PICHA: Man United wapoteza nyumbani dhidi ya Barcelona Champions League

Baada ya kusubiriwa kwa hamu kwa zaidi ya wiki mbili na mashabiki wa soka, hatimae usiku wa April 10 2019 katika uwanja wa Old Trafford ulichezwa mchezo wa Man United dhidi ya FC Barcelona, huo ukiwa ni mchezo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League msimu wa 2018/2019 kwa timu hizo.

Huo ulikuwa ni mchezo wenye shauku kubwa kwa mashabiki wa Man United kwa sababu walitaka kujua na kuona timu yao ikilipa kisasi kwa FC Barcelona, baada ya kupoteza fainali mbili ya UEFA Champions League dhidi ya miamba hiyo ya Nou Camp.

Barcelona wameendeleza kuwa wababe baada ya kumfunga Man United kwa goli 1-0 lilipatikana kwa Luke Shaw kujifunga baada ya Luis Suarez kupiga kichwa alichopigiwa krosi na Lionel Messi dakika ya 12 ya mchezo, Man United kama wanataka kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo watalazimika kwenda Nou Camp wiki ijayo kupata ushindi wa kuanzia magoli 2-0, au 2-1 na kuendelea.

Spurs wameiua Man City, FC Porto hawajatoka salama Anfield

Game za mzunguuko wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League zimechezwa jana nchini England, usiku wa April 9 zimechezwa game mbili ambazo zilikuwa zinakutanisha timu tatu za England, Man City alikuwa ugenini kucheza dhidi ya Tottenham wakati Liverpool alikuwa nyumbani Anfield kuikaribisha FC Porto ya Ureno.
Mchezo wa Man City dhidi ya Tottenham ulimalizika kwa Tottenham kupata ushindi wa goli 1-0 lililofungwa na Heung-Min Son dakika ya 78, wakati Liverpool nao wakiilaza FC Porto kwa magoli 2-0 yaliofungwa na Naby Keita dakika 5 na Firmino dakika ya 26 ya mchezo.

England ambao ndio wanakutanisha timu nyingi katika hatua hii ya robo fainali wakiingiza jumla ya timu nne (Tottenham, Liverpool, Man City na Man United) watalazimika kuziombea dua timu zao hili zifanye vizuri katika hatua hiyo japo moja italazimika kuishia hatua ya robo fainali 100% (Man City na Tottenham) kwa kukutana wenyewe kwa wenyewe, mechi za April 10 ni Man United dhidi ya FC Barcelona na Ajax dhidi ya Juventus.