Msimamo wa Epl baada ya mechi za leo


Msimamo wa Epl baada ya mechi za leo


Sasa rasmi Simba Sc itavaana na klabu anayoichezea mtanzania Hassan Kessy Nkana Fc katika hatua ijayo ya mtoano ya ligi ya mabingwa Afrika #sokaUpdates
Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba muda mfupi ujao wa wanashuka dimbani huko Eswatini kuikabili Mbabane Swallows katika mchezo wa marudiano wa ligi ya mabingwa.
Hiki hapa kikosi cha Simba kinachoanza mchezo huo;
Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba muda mfupi ujao wa wanashuka dimbani huko Eswatini kuikabili Mbabane Swallows katika mchezo wa marudiano wa ligi ya mabingwa.
Hiki hapa kikosi cha Simba kinachoanza mchezo huo;
Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba kimeondoka leo Jumapili kuelekea nchini Afrika Kusini ambako kitaunganisha kwenda Eswatini kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa ligi ya mabingwa barani Afrika.
Msafara wa mabingwa hao wa kihistoria umejumuisha wachezaji 20 na viongozi nane wa benchi la Ufundi.
Mchezo dhidi ya Mbabane Swallows utapigwa siku ya Jumatano, Disemba 05 huko eSwatini (zamani Swaziland)
Afisa Habari wa Simba Haji Manara amesema wanakwenda kuivaa Mbabane Swallows kwa tahadhari kubwa huku wakifahamu wanahitaji kufuzu kwenda raundi inayofuata.
Jumatano Simba itashuka dimbani ikiwa na faida ya ushindi wa mabao 4-1 iliyopata mapema wiki hii kwenye dimba la Taifa.



















Mrisho Ngasa ni kama amezaliwa upyaaaa kwani mambo anayofanya dimbani sio ya kawaida. Leo amefunga bao lake la nne msimu huu akitupia katika michezo miwili mfululizo.
Anachokifanya Ngasa sasa ni kuwapa majibu ‘mbashara’ wale wote waliokuwa wanam-beza na kusema umri umemtupa mkono.
Amekuwa na ushirikiano mzuri sana na Heritier Makambo ambaye kasi yake ya kupachika mabao tayari imeanza kuwatia hofu upande wa pili
Amefikisha mabao saba na inaonekana atafunga sana msimu huu.
Makambo ni mshambuliaji aliyekamilika, amedhihirisha hilo na anao uwezo wa kufunga aina zote za mabao.
Kwa hakika kikosi cha Yanga sasa kimeiva.
Licha ya changamoto za nje ya uwanja, wachezaji wa Yanga wamekuwa wakicheza kwa kujituma, Na sasa kuna kitu kingine kimeongezeka, WANAJIAMINI
Ile burudani ya ‘kampa-kampatena’ imeanza kurejea. Sasa Yanga inapata ushindi huku pia ikicheza mpira ‘mwingi’ tofauti na ilivyokuwa mwanzoni mwa msimu
Yanga hii itawashangaza wengi msimu huu..