Category: simba
Hiki hapa Kikosi cha Simba kitakacho cheza leo dhidi ya JKT Tanzania
Kikosi cha Simba dhidi ya JKT Tanzania leo
2. Nicolas Gyan
3. Asante Kwasi
4. Yusuf Mlipili
5. Juuko Murshid
6. Said Ndemla
7. Hassan Dilunga
8. Jonas Mkude
9. Adam Salamba
10. John Bocco (c)
11. Clatous Chama
2. Erasto Nyoni
3. Paul Bukaba
4. James Kotei
5. Rashid Juma
6. Meddie Kagere
7. Emmanuel Okwi
Okwi, Chama hawakugoma – Manara

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya klabu ya Simba yaliyopo mtaa wa Msimbazi, Manara amesema klabu iliwapa ruhusa wachezaji hao kushughulikia masuala yao ya kifamilia na tayari wamesharipoti mkoani Morogoro kujiunga na wenzao
“Hakuna mchezaji aliyegoma kama taarifa zinavyoenezwa huko mitandaoni hivi timu inayocheza klabu bingwa Africa kuna mchezaji anaweza kugoma?”, amehoji Manara
“Okwi na Chama walipewa ruhusa maalum na tayari wapo kambini toka jana”
“Sisi kwa sasa tunaweza chukua mchezaji yeyote hata Tp Mazembe sio kama kipindi kile kwa sasa simba ni giant inabeba yeyote”
“Tuna barua zaidi ya 100 za wachezaji mbalimbali wameomba kuchezea Simba msimu ujao tena wengine wametoka vilabu vikubwa hapa Tanzania wanahitaji kucheza hata bure”
Wasauzi wampagawisha Okwi,aanza mbwembwe

Mkataba wa Okwi unatarajiwa kumalizika ndani ya siku 60 huku mchezaji huyo raia wa Uganda akionyesha dalili zote za kutaka kuondoka Msimbazi
Okwi anahusishwa na vilabu kadhaa vinavyoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini, Orlando Pirates na Kaizer Chiefs
Kocha Patrick Aussems alimuondoa Okwi katika kikosi kilichokwenda mkoani Morogoro baada ya mchezaji huyo kuchelewa kuripoti kambini
Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema hana taarifa kuhusu mshambuliaji huyo ambaye alikuja nchini na kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda Cranes na alicheza mchezo dhidi ya Stars
“Mimi sijui chochote kuhusiana na Okwi labda waulizwe viongozi wangu wa juu, hayupo kwenye msafara wetu huu unaoelekea Morogoro, hivyo waulizwe viongozi wa juu suala lake,”Rweyemamu alinukuliwa na Championi jana
Hata hivyo Okwi amekuwa na kawaida ya kuchelewa kuripoti kambini kila anapotoka kutimiza majukumu ya timu ya Taifa
Hali ni tofauti kwa Juuko Murshid ambaye tangu aliporejeshwa kikosini, amekuwa akiwajibika ipasavyo
Juuko alikuwa miongoni mwa wachezaji waliowahi kuripoti kambini baada ya kumalizika michezo ya AFCON
Taarifa zilizopatikana mapema leo zimebainisha Okwi amerejea na ameshatua mkoani Morogoro kuungana na wenzake
Manara kuweka hadharani mkakati wa kuimaliza TP Mazembe


Okwi, Chama waongeza nguvu Simba ikijiandaa kuikabili JKT Tanzania

Okwi na Chama hawakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kilichoifumua Mbao Fc mabao 3-0 baada ya wachezaji hao kuchelewa kurudi kutoka nchini kwao walikokwenda kutimiza majukumu ya timu ya Taifa
Baada ya mchezo wa kesho, Simba itaendelea kubaki mkoani Morogoro kuendelea na maandalizi ya mchezo wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe
Mchezo huo utapigwa Jumamosi, April 06 kwenye uwanja wa Taifa
Simba vs JKT Tanzania kupigwa Jumatano

Licha ya kukabiliwa na mchezo wa robo fainali ligi ya mabingwa siku ya Jumamosi, April 06 dhidi ya TP Mazembe, TFF imegoma kusogeza mbele mchezo dhidi ya JKT Tanzania ambao utapigwa April 03 2019 kama ulivyopangwa
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema kwa sasa wanaelekeza nguvu zao kuelekea mchezo huo kabla ya kuanza maandalizi ya mchezo dhidi ya TP Mazembe
“Nitalazimika kubadili kikosi ili kila mchezaji apate nafasi kwani baada ya mchezo huo tutakuwa na siku mbili tu za kujiandaa kabla ya kuivaa TP Mazembe,” amesema
Akizungumzia ushindi wa mabao 3-0 ambao Simba ilipata jana dhidi ya Mbao Fc, Aussems alisema mipango yao ni kuhakikisha wanashinda kila mchezo ili waweze kutetea ubingwa hivyo ushindi huo unaendelea kuweka hai mipango yao
“Kila mechi tunacheza kushinda, hata huu mchezo tulistahili kushinda, tulianza kushambulia tangu mwanzo hadi mwisho, mchezo ulikuwa mgumu lakini tulitengeneza nafasi”
SIMBA 3-0 MBAO FC

Mabao mawili ya nahodha John Bocco na moja la Meddie Kagere yametosha kuihakikishia Simba ushindi muhimu ambao umewasogeza karibu ya Azam Fc inayoshika nafasi ya pili baada ya kufikisha alama 57
Azam Fc ina alama 59 hata hivyo Simba ina michezo sita mkononi hivyo ni suala la muda tu mnyama atakaa katika nafasi yake na hatimaye kutetea ubingwa waliotwaa msimu uliopita
Mabao mawili aliyofunga Bocco leo yamemfanya afikishe mabao 11 akihitaji kufunga bao moja tu kumfikia Heritier Makambo wa Yanga
Kagere amezidi kumkaribia Salim Aiyee wa Mwadui Fc mwenye mabao 16, baada ya bao lake la mkwaju wa penati alilofunga leo kumfanya afikishe mabao 14
Baada ya ushindi wa leo kikosi cha Simba kitaendelea na maandalizi ya mchezo wa robo fainali ligi ya mabingwa dhidi ya TP Mazembe
Simba itaendelea kujifua mkoani Morogoro kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa April 06 katika dimba la Taifa
Bocco, Kagere kuongoza maangamizi ya Mbao Fc leo

Baada ya kufanya kazi kubwa ya kuivusha Simba hatua ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa dhidi ya AS Vita, kisha akaivusha Stars fainali za AFCON 2019 katika mchezo dhidi ya Uganda kwa kutengeneza mabao mawili kati ya matatu yaliyofungwa na Stars, Bocco leo atakuwa dimbani kufanya kazi maalum ya kuitafutia Simba alama tatu muhimu
Aidha kinara wa upachikaji mabao katika kikosi cha Simba, Meddie Kagere naye atakuwa na nafasi ya kuongeza mabao yake na kumkaribia Salum Aiyee wa Mwadui Fc mwenye mabao 16
Kagere yuko nafasi ya pili kwenye orodha ya vinara wa upachikaji mabao akiwa na mabao 13
Bocco na Kagere wamerejea kikosini baada ya kutumikia timu zao za Taifa wakiwa ‘fit’ na hakuna shaka Aussems anazihitaji silaha hizi kuweza kuimaliza Mbao Fc baadae leo
Wadau wa Simba Morogoro wapongezwa kwa ukarabati uwanja wa Jamhuri

Katika kuhakikisha uwanja huo unakuwa na hali nzuri, wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba mkoani Morogoro walijitolea kuufanyia ukarabati
Ukarabati uliofanywa ni pamoja na kun’goa magugu, kujaza vifusi sehemu zenye mashimo na kuotesha nyasi pamoja na kumwagilia katika kipindi cha wiki tatu zilizopita
Pia ukarabati umefanywa kwenye vyoo na vyumba vya kubadilishia nguo
Meneja wa uwanja huo John Simkoko amewapongeza Wanasimba kwa jitihada zao za kuuboresha uwanja huo
Simba itaanza rasmi kuutumia uwanja wa Jamhuri kama uwanja wake wa nyumbani kesho Jumapili itakapochuana na Mbao Fc katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara









