Kamati Maalum Yanga kutua Bungeni, kutambulishwa Dodoma

Kesho tarehe 05/04/2019, Kamati maalumu iliyoundwa ili kuhamasisha uchangiaji Yanga inayoongozwa na Mwenyekiti Mh. Anthony Mavunde itafika bungeni kutambulishwa

Tarehe 06/04 kutafanyika uzinduzi rasmi wa kuichangia Yanga.

Tukio hilo la aina yake litaanza saa 12:00 jioni katika ukumbi wa Morena Hotel iliyopo Dodoma huku likiwa mubashara Azam 2 Tv, Kiingilio hakikisha umevaa jezi ya Yanga tu.

Wasanii wafuatao wapenzi wa Yanga watakuwepo makao makuu ya nchi ili kuratibu shughuli hiyo, Mhogo Mchungu, Mr Blue, Msaga Sumu, Single Mtambilike, Wema Sepetu, Haji Mbotto, Rado, Riyama, Uwoya, Madee, Papii Kocha, Ray Kigosi, Frola Mvungi, Kajala Masanja, Barafu, Chopa Mchopanga.

Wengine ni Kalapina, Rich One, Batuli, Haji Adam, Jacqueline Wolper , Yussuf Mlela ,Stamina,Esha Buheti, Steve Nyerere, Chuchu Hans, Dude, Shamsa Ford, Johari, mtangazaji Zamaradi Mketema, MC Pilipili, Seneta Msungu!

Hafla hiyo ya uzinduzi pia itahudhuriwa na watu maarufu na mashuhuri katika medani tofauti

Zahera aahidi ushindi mchezo dhidi ya Ndanda Fc

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera leo atakiongoza kikosi cha timu yake kuikabili Ndanda Fc katika mchezo wa ligi kuu utakaopigwa uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara

Akizungumzia maandalizi ya kikosi chake, Zahera amesema baada ya kufanya mazoezi kwa takribani siku mbili Mtwara, vijana wake wako tayari kwa ajili ya mchezo wa leo

“Nafurahi tumefanya maandalizi mazuri. Wachezaji hawakupata matatizo tangu tulipowasili hapa Mtwara,” amesema

“Hali ya hewa ni joto sawa na Dar es salaam, hivyo haiwezi kuwa changamoto kwetu

“Juzi jioni tulifanya mazoezi ya kuondoa uchovu jana pia tulifanya mazoezi mepesi ya kunyoosha minofu. kikosi changu kipo sawa kuelekea mchezo wa leo”

Yanga inasaka ushindi muhimu leo ili iendelee kuchimbia kileleni mwa msimamo wa ligi

Kipenga kimepulizwa, fomu za uchaguzi Yanga zaanza kutolewa

Baada ya ‘figisu’ za uchaguzi kumalizika, hatimaye Wanayanga wana uhakika sasa kuwa mwezi ujao uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo utafanyika na viongozi wapya watapatikana katika nafasi zote

Jana Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF Malangwe Mchungahela aliweka wazi kuwa uchaguzi utafanyika May 05 badala ya April 28 kutokana na siku hiyo kutakuwa na mchezo wa fainali za AFCON U17. Uchaguzi huo utasimamiwa na Yanga, wao TFF watakuwa waangalizi tu

Tayari kipenga kimepulizwa na leo fomu zinaanza kutolewa Makao Makuu ya klabu Mtaa wa Twiga na Jangwani jijini Dar es salaam

Hii ni nafasi adhimu kwa Wanayanga kuijenga timu yao upya baada ya mateso ya takribani misimu miwili

Ni wakati kwa Wanachama wenye sifa na uwezo wa kuipeleka Yanga mbele kujitokeza kuchukua fomu

Aidha si vibaya kwa wanachama wengine kushawishiwa wachukue fomu kugombea pale tunapoona wanazo sifa na tuna imani nao

Huu ni wakati wa kuijenga Yanga imara ambayo itakuwa na mafanikio zaidi

Wanachama wajitokeze kwa wingi kuchukua fomu na siku ya uchaguzi, haipaswi kufanya makosa kwa wapiga kura.

Wanachama watumie muda wao kuwasikiliza wagombea wote wakati wa kampeni ili waweze kuchagua viongozi ambao wataweza kuitoa Yanga hapa ilipo

Maelezo zaidi jinsi ya kuchangia Yanga

Kwa wanaotumia MPESA maelezo haya hapa chini jinsi ya kuchangia Yanga.

Pia wachangiaji wanaweza kutuma michango yao moja kwa moja kwenda Akaunti ya CRDB ya Yanga : 0150419775800

TIGOPESA

1. Bonyeza *150*01#
2. Chagua Lipa Bili
3. Chagua Ingiza namba ya kampuni
4. Andika 101120
5. Sehemu ya kumbukumbu namba andika 1
6. Weka kiasi (2,500 na kuendelea)
7. Andika namba yako ya siri kuhakiki malipo yako

Lipuli watapata tabu sana – Zahera

Baada ya kupenya hatua ya nusu fainali michuano ya kombe la FA (ASFC), kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema mchezo wa nusu fainali dhidi ya Lipuli Fc utakuwa mwepesi, ana matumaini makubwa kuwa kikosi chake kitatinga fainali

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo jana, Zahera amesema mchezo dhidi ya Alliance ulikuwa mgumu sana na walihitaji bahati kuweza kusonga mbele

“Leo (jana) tumeteseka sana, michezo miwili tuliyocheza na Alliance hapa Mwanza tumeteseka sana lakini mchezo ujao dhidi ya Lipuli utakuwa rahisi kwetu,” alisema Zahera

“Nimewaangalia Lipuli Fc, mchezo waliotufunga tuliwazidi kila kitu lakini tulikosa bahati tu”

“Ukiacha mpira wa adhabu waliyofunga na kona moja aliyodaka Kindoki, hawakutengeneza nafasi zaidi yetu”

“Sisi tulitengeneza nafasi sita lakini hatukuzitumia. Hivyo Lipuli Fc hawatutishi, tutarejea Iringa kucheza nao “

Yanga inatarajiwa kucheza na Lipuli Fc mwishoni mwa mwezi wa nne katika mchezo wa nusu fainali utakaopigwa uwanja wa Samora, Azam Fc itacheza na KMC katika mchezo mwingine wa nusu fainali utakaopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi

FT : Alliance 1-1 Yanga, mikwaju ya penati 4-3 yaipeleka Yanga nusu fainali

Mabingwa wa kihistoria Tanzania, Yanga wametinga nusu fainali ya kombe la FA (ASFC) baada ya kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penati 4-3 kufuatia matokeo ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Alliance Fc


Yanga ilitangulia kupata bao la kuongoza kwenye dakika ya 39 likiwekwa kambani na Heritier Makambo kwa kombora la nje ya 18
Alliance Fc iliyokuwa kwenye kiwango bora ilisawazisha bao hilo kwenye dakika ya 62 kupitia kwa Joseph James
Baada ya kumalizika kwa dakika 90 huku matokeo yakiwa 1-1, changamoto ya mikwaju ya penati ikatumika kuamua mshindi

Deus Kaseke, Paulo Godfrey, Thabani Kamusoko na Haruna Moshi ndio waliofunga penati za Yanga
Yanga sasa itachuana na Lipuli Fc kwenye mchezo wa nusu fainali

Kikosincha Yanga vs Alliance FC

1. Klaus Kindoki

2. Paulo Godfrey

3. Gustavo Simon

4. Said Juma

5. Kelvin Yondani

6. Feisal Salum

7. Mrisho Ngasa

8. Papi Tshishimbi

9. Heritier Makambo

10. Amissi Tambwe

11. Pius Buswita

SUB

Ibrahim Hamid

Jaffar Mohammed

Andrew Vicent

Haruna Moshi

Thabani Kamusoko

Raphael Daudi

Deus Kaseke

Yanga yajifua Mwanza tayari kuikabili Alliance Fc

Kikosi cha Yanga jana jioni kilifanya mazoezi kwenye uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba kujiandaa na mchezo wa robo fainali kombe la FA (ASFC) dhidi ya Alliance Fc

Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa CCM Kirumba

Vinara hao wa ligi kuu ya Tanzania Bara walitua jana asubuhi jijini Mwanza wakiongozwa na kocha Mwinyi Zahera

Jioni ya leo Ijumaa Yanga inatarajiwa kufanya mazoezi yake ya mwisho kwenye dimba la CCM Kirumba tayari kwa mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na wakazi wa jiji la Mwanza na maeneo ya jirani

Zahera ataja sababu ya kumuacha Ajib Dar

Nahodha wa kikosi cha Yanga Ibrahim Ajib hajasafiri na timu hiyo kuelekea mkoani Mwanza ambapo keshokutwa Jumamosi itashuka katika uwanja wa CCM Kirumba kuikabili Alliance Fc kwenye mchezo wa robo fainali, kombe la FA

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema Ajib hakujumuishwa katika kikosi kwa kuwa bado hajawa ‘fit’ tangu apone majeraha ya misuli

Zahera amesema Ajib anahitaji muda zaidi wa kufanya mazoezi ili aweze kuwa tayari kurejea dimbani

Akizungumzia mchezo huo, Zahera amesema wamejiandaa kikamilifu kuikabili Alliance Fc ambayo inaonekana kupania zaidi mchezo huo

“Tunaufahamu ubora wa Alliance Fc na hata udhaifu wao pia tunaujua, hatuna wasiwasi kuelekea mchezo huo,” amesema Zahera

Mcongoman huyo aliyerejea usiku wa kuamkia jana na kuungana moja kwa moja na kikosi cha Yanga, amesema atatumia siku ya leo na kesho kufanya maandalizi ya mwisho tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumamosi March 30 katika dimba la CCM Kirumba