MO DEWJI APONGEZA UBINGWA SIMBA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Mohammed Dewji ‘Mo’ ameipongeza timu hiyo kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara kwa msimu wa pili mfululizo

Mo amesema mafanikio hayo yamepatikana kutokana na juhudi zilizofanywa na wachezaji, benchi la ufundi, viongozi na wadau wote wa klabu ya Simba kila mmoja kwa nafasi yake

“Mungu mkubwa. Pongezi kwa wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, wanachama, mashabiki, na wapenzi wote wa SIMBA, tumeshinda! Najivunia mafanikio haya,” amesema Mo

Naye Msemaji wa Simba Haji Manara amewapa shukrani za kipekee wachezaji, benchi la ufundi pamoja na mashabiki wa timu hiyo kwani wamekuwa na mchango mkubwa kwa mafanikio ya Simba msimu huu

“Tumshukuru Mungu muweza aliyetaka Simba iwe Bingwa tena”

“Tuwapongeze sana Wachezaji wetu wote, Benchi la ufundi chini ya kocha Patrick Aissems, lakini kipekee tuwashukuru nyie Wanachama na Washabiki wetu ambao mimi nnaamini ndio chachu ya huu ubingwa”

“Kwangu shujaa wa kwanza Simba ni Mshabiki wetu, Tunawashukuru sana”

Simba imetwaa ubingwa leo baada ya kuifunga Singida United mabao 2-0

Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa baada ya kufikisha alama 91 kwenye msimamo wa ligi

Alama hizo haziwezi kufikiwa na timu nyingine yoyote katika michezo iliyobaki

Simba imeibuka na ubingwa huku ikiwa na michezo miwili mkononi

BREAKING NEWS: SIMBA WATWAA UBINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA 2018/2019

Simba imefanikiwa kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Singida United mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Namfua
Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa wake wa 20
Simba imefikisha alama 91 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine hata kama zitashinda michezo yote iliyobaki

Wachezaji, benchi la Ufundi na viongozi wa Simba wanastahili pongezi kwa mafanikio haya ya kikosi cha Simba

Ubora wa timu, ushirikiano baina ya Wana Msimbazi ndio sababu kubwa iliyopelekea kuibuka na ubingwa wa pili mfululizo

Msimu haukuwa mwepesi kutokana na Simba kushiriki katika mashindano mengi, lakini juhudi za wachezaji zimewezesha kupatikana kwa mafanikio haya
Simba imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao, mashindano ambayo tayari imepata uzoefu mkubwa msimu baada ya kufika hatua ya robo fainali
Hongera kwa wanamsimbazi

SIMBA BINGWA LIGI KUU TANZANIA 2018/2019

Simba imefanikiwa kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo baada ya leo kuichapa Singida United mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Namfua

Mabao ya Meddie Kagere na John Bocco yalitosha kuihakikishia Simba ubingwa wake wa 20

Simba imefikisha alama 91 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine hata kama zitashinda michezo yote iliyobaki

Wachezaji, benchi la Ufundi na viongozi wa Simba wanastahili pongezi kwa mafanikio haya ya kikosi cha Simba

Ubora wa timu, ushirikiano baina ya Wana Msimbazi ndio sababu kubwa iliyopelekea kuibuka na ubingwa wa pili mfululizo

Msimu haukuwa mwepesi kutokana na Simba kushiriki katika mashindano mengi, lakini juhudi za wachezaji zimewezesha kupatikana kwa mafanikio haya

Simba imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu ujao, mashindano ambayo tayari imepata uzoefu mkubwa msimu baada ya kufika hatua ya robo fainali

Hongera Wachezaji, Hongera Benchi la Ufundi, Hongera Viongozi, Hongera Mashabiki wa Simba……!

SHEREHE ZA UBINGWA SIMBA KUANZA LEO SINGIDA

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wako mkoani Singida ambapo leo watashuka katika uwanja wa Namfua kuikabili Singida United katika mchezo ambao huenda wababe hao wa soka la Tanzania watatawazwa mabingwa

Simba inayoongoza ligi ikiwa na alama 88, inahitaji alama moja tu katika mchezo huo ili iweze kurudi na kombe jijini Dar es salaam

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wataingia katika mchezo huo kusaka ushindi ingawa wanafahamu pointi moja itatosha kutimiza lengo la kutwaa ubingwa

“Tuko hapa kwa ajili ya kusaka ushindi, Nawakaribisha mashabiki wetu waje kwa wingi uwanjani kutuunga mkono ili tuweze kutimiza lengo la kutwaa ubingwa leo,” amesema Aussems

SEVILLA : Kutua Na Msafara wa watu 60

Timu ya Sevilla kutoka Hispania inatarajiwa kuwasili leo ikiwa na msafara wa watu 60 unaojumuisha wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa timu hiyo

Sevilla ambayo itacheza na Simba mchezo wa kirafiki keshokutwa, ikiwa nchini itashiriki katika shughuli za kijamii

Safari ya Sevilla nchini imedhaminiwa na kampuni a SportPesa ambao pia ni wadhamini wakuu wa timu za Simba na Yanga

Mabingwa hao wa kihistoria wa taji la Europa, wanakuwa timu ya kwanza kutoka ligi kuu ya Hispania kutembelea Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla

Sevilla iliyotwaa taji la Europa mara tano, itacheza na Simba keshokutwa Alhamisi, May 23 katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa, saa moja jioni

TETESI ZA USAJILI SIMBA LEO JUMANNE

Tetesi za usajili Simba leo 21 May 2019

Kikosi cha Simba leo huenda kikatangaza ubingwa kikicheza kwenye ardhi ya Singida katika uwanja wa Namfua, Simba inahitaji walau sare tu ili kuweza kutangaza Ubingwa mbele ya Singida United wanaohitaji ushindi ili kujihakikishia kuendelea kusalia ligi kuu.

Ukiachana na hayo ya Simba kushinda inaelezwa kuwa kikosi cha Simba kinaendelea kutafuta wachezaji wakuimarisha kikosi chao kwaajili ya msimu ujao.

Kama ulijisahaulisha, mchezaji Vitalis Mayanga wa Ndanda inaelezwa kuwa ni suala la muda tu kutua Simba kwani Simba na Ndanda walishamalizana muda tu na kijana anasubiri ligi iishe waweze kumjumuisha kikosini.

Vitalis Mayanga licha ya kuwa akitajwa kuwaniwa na baadhi ya vilabu nchini Tanzania Yanga ikitajwa lakini imebainika ni mchezaji halali wa Simba anayesubiria ligi iishe aungane na mabingwa hao wa soka nchini.
Credit: Kwataunit

MATOKEO YA MECHI ZA JANA JUMATATU.

MATOKEO YA MECHI ZA JANA JUMATATU.
Serie A
FT 3 Lazio
3 Bologna
Ligi Kuu Bara.
FT 2 Biashara United
1 Ruvu Shooting
:
RATIBA YA MECHI ZA LEO:
– Ligi kuu Bara
16:00 Mbao FC
KMC FC
16:00 Singida United
Simba SC
.
– Egypt Premier League
23:00 Al Masry
El Entag El Harby
23:00 El Geish
Al Ittihad
23:00 ENPPI
Misr Lel Makasa
23:00 Smouha
Petrojet
23:00 Wadi Degla
Haras El Hodood
.
– International – Club Friendlies.
19:30 Beitar Jerusalem
Atletico Madrid
#Updates #sokawaytz